Sikieni neno la Mungu wetu, zileteni zaka kwa hazina
Leteni na mioyo yenu yote; mibaraka itakuja.
Zileteni zaka kwa hazina, kanijaribu sasa nazo;
Nitakupeni mibaraka, zaidi ya nafasi ya kupewa.
Wakati Roho Mtakatifu kwako? Uzilete zaka kwa hazina
Ukae karibu na Bwana wako, ndipo utabarikiwa.
Je,una kasoro na Bwana wako? Uzilete zaka kwa hazina,
Uzilete kama alivyo sema, Ndipo utabarikiwa.
Ushukuru Bwana na moyo wote, unapo leta zaka ghalani;
Usadiki ahadi zake zote, ndipo utabarikiwa.
Tuimbe sote nyimbo za furaha, tunapoleta zaka ghalani
Twimbe kabisa na furaha kubwa, kwani tutabarikiwa.
Comments