Nimetunukiwa tuzo lenye thamani, nimeletewa zawadi toka mbinguni, nimejishindia Mwana wa Mungu nimepewa Yesu zawadi tosha x2
Ninashangilia naimba kwa furaha, ninarukaruka nacheza kwa furaha. Napiga makofi na vigelegele, nimempata Yesu tuzo la ajabu…mimi
Ninakushukuru ee Mungu Baba Yesu, nasema asante kwa mema yako yote, Napiga filimbi ngoma na kayamba, nimejishindia Bwana wa Bwana…mimi
Nikiwa na Yesu magonjwa yamepona, nikiwa na Yesu mashaka yamekwisha, Yesu kiongozi Yesu Jemedari, Yesu mchungaji Yesu mambo yote…mimi
Maisha marefu nituzo nimetuzwa, uzima milele nimeshaahidiwa, Mbinguni kwa Baba nitakaribiswa, nitaishi vyema siku zangu zote…mimi
Comments