top of page

Yesu nipendaye

Yesu unipendaye kwako nakimbilia,

Ni wewe utoshaye mwovu akinijia.

Yafiche ubavuni mwako maisha yangu;

Nifishe bandarini, wokoe moyo wangu.


Ngome nyingine sina; nategemea kwako,

Usinitupe Bwana, nipe neema yako,

Ninakuamania, kuniweshesha;

Shari wanikingia, vitani wanitosha.


Nakutaka mpaji, vyote napata kwako;

Niwapo muhitaji, utanijazi vyako;

Nao waangukao wanyonge wape nguvu;

Poza wauguao, uongoze vipofu.


Bwana umeniosha moyo kwa damu yako;

Neema ya kutosha yapatikana kwako;

Kwako Bwana naona kisima cha uzima;

Mwangu moyoni, Bwana, bubujika daima.

10 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page