Yesu nakupenda, u mali yangu, Anasa za dhambi sitaki kwangu:
Na mwokozi aliyeniokoa Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Moyo umejaa mapenzi tele Kwa vile ulivyonipenda mbele,
Uhai wako ukanitolea Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Ulipoangikwa msalabani Tusamehewe tulio dhambini;
Taji ya miiba uliyoivaa, Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Mawanda mazuri na masikani Niyatzamapo huko mbinguni,
`Tasema na taji nitakayovaa, Sasa nakupenda, kuzidi pia.
Comments