top of page

Yesu nakupenda

1. Yesu nakupenda, U Mali yangu,

anasa za Dhambi sitaki kwangu;

Na Mwokozi aliyeniokoa,

Sasa nakupenda, kuzidi Pia.


2. Moyo umejaa Mapenzi tele,

kwa vile ulivyonipenda mbele,

Uhai Wako ukanitolea,

Sasa nakupenda, kuzidi pia.


3. Ulipoangikwa Msalabani,

tusamehewe tulio dhambini;

Taji ya miiba uliyoivaa,

sasa nakupenda, kuzidi pia


4. Niwapo hai, niwapo maiti,

kupendana nawe kamwe siachi;

Hari za kifo zikinienea,

sasa nakupenda, kuzidi pia.


5. Mawanda mazuri, na masikani,

niyatazamapo huko Mbinguni,

Tasema na taji nitakayovaa, sasa

nakupenda, kuzidi pia.

5 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page