Yesu mwema najitolea kwako Kwa leo hii na siku zote
Nafsi yangu na moyo wangu wote
Heri kweli, heri kweli Heri kweli raha ya uwingu x2
Ndani mwangu umekuja daima Kuwa nami ni upendo wako
Ewe mpenzi mwenye utamu mwingi
Ni mapendo, ni mapendo ni mapendo ya moyo wako x2
Nitaweza kukurudishia nini Kwa wema huu na pendo lako
Roho yangu umeifadhilia
Nikupende, nikupende nikupende ni tamaa yangu x2
Weka Rabi katika roho yangu Wema wako na unyenyekevu
Na pendo kuu fadhila na amani
Niongoze, niongoze niongoze katika amani x2
Comments