Yesu aliniita, ‘Njoo, Raha iko kwangu,
Kichwa chako ukilaze kituani mwangu.‘
Nilikwenda kwake mara, Sana nilichoka;
Nikapata kwake raha na furaha.
Yesu aliniita, ‘Njoo, Kwangu kuna maki:
Maji ya Uzima, bure, unywe uwe hai.‘
Nilikwenda kwake mara na maji nikanywa:
Naishi kwake na kiu kamwe sina tena.
Yesu aliniita, ‘Njoo, Dunia i giza,
Ukinitazama, nuru `takungarizia.‘
Nilikwenda kwake mara, Yeye jua langu,
Ni kila wakati mwanga safarini mwangu.
Comments