Nendeni na amani, misa imekwisha Nendeni mkayatangazeni yote mliyoyasikia Katika masomo injili na mahubiri. Tazama Kristu Bwana yupo nasi daima- Daima mpaka ukamilifu wa dahari
Neema na baraka mlizozipata Zikae nanyi siku zote
Ishi kwa upendo amani umoja matunda ya Ekaristia
Na yahubirini mliyoyasikia kwa matendo na miendo yenu
Comentários