UTUKUFU
SOL: Utukufu kwa Mungu juu
Na amani duniani yote.
ALL: Kwa watu wenye mapenzi (mema) x 2
1. Twakusifu twakuheshimu, twakuabudu, twakutukuza,
All: Mungu wa majeshi ewe Baba x 2
2. Twakushukuru Mfalme, wa mbingu Mungu Baba yetu
All: Mungu wa majeshi ewe Baba x 2
3. Ufutaye dhambi zetu tuhurumie tusikilize
All: Mungu wa majeshi ewe Baba x 2
4. Uketiye kuume kwa Baba, upekee yako Yesu kristu
All: Mungu wa majeshi ewe Baba x 2
5. Naye roho mtakatifu, katika utukufu wa Baba
All: Mungu wa majeshi ewe Baba x 2
NASADIKI
Nasadiki kwa Mungu mmoja Nasadiki x 2
Mimi kweli nasadiki mimi - Nasadiki x 2
Ndiye Baba mwenyezi Nasadiki x 2
Mwumba mbingu na dunia - Nasadiki x 2
Na kwake Yesu kristu Nasadiki x 2
Nasadiki kwa Mungu mmoja Nasadiki x 2
1. Mwanaye wa pekee
Atokaye kwa baba
Kazaliwa na Bikira
Kwa roho mtakatifu.
2. Kisha akasulubiwa
Kwa amri ya pilato
Akafa na kazikwa
Kashukia kuzimu
3. Yeye akafufuka
Kapaa juu mbinguni
Kaketi kuume kwake
Mungu Baba mwenyezi
4. Tarudi kuhukumu
Wazima pia wafu.
Kwa roho mtakatifu
Kanisa katoliki
5. Shirika takatifu
‘Ndoleo la dhambi zetu
Nangojea ‘fufuko
Uzima wa milele.
MTAKATIFU
Mtakatifu Bwana – Ee Mungu wa majeshi x 2
Mbingu na dunia – Ee zimejaa utukufu x 2
Hosana – juu mbinguni x 2
Hosana juu mbinguni.
Mbarikiwa yeye – Ajaye kwa jina la Bwana x 4
FUMBO LA IMANI
Kristu alikufa
Kristu alifufuka
Kristu atakuja – atakuja tena x 2
AMINA
Amina A – amina – Amina A – amina x 2
Amina – A – amina x 2
Amina – A – amina x 2
BABA YETU
Baba yetu uliye juu mbinguni - Baba
Jina lako Ee Baba nalo nalitukuzwe - Baba
Ufalme wako nao ufike Baba
Utakalo Ee Baba kweli nalifanyike - Baba
Baba yetu Baba x 3 ) x 2
Duniani Ee Baba kama Mbinguni - Baba
Tupe leo mkate wetu wa kila siku - Baba
Tusamehe Ee Baba makosa yetu - Baba
Kama vile twasamehe waliotukosea - Baba
Situtie Ee Baba majaribuni - Baba
Walakini Ee Baba utuopoe - Baba
Maovuni Ee Baba utuopoe - Baba
Maovuni Ee Baba kweli utuopoe - Baba
Kwa kuwa ufalme ni wako Baba - Baba
Na nguvu vyoteni vyako - Baba
Utukufu Ee Baba hata milele - Baba
Utukufu Ee baba kweli hata milele - Baba
Comments