top of page

Wimbi Litakasalo

Wimbi la damu ya Yesu Linatutakasa;

Aliumia kusudi Tupate uzima.


Wimbi la damu naona, Naingia, natakaswa!

Bwana asifiwe sana, Hutakasa, hutakasa.


Damu inasema kwangu, Nasikia mvuto;

Inasema, moyo wangu Hutakaswa nayo.


Naondoka kutembea Kwa nuru ya mbingu;

Mavazi yamesafishwa; Moyoni ni Yesu.


Neema ni ya ajabu, Kutakaswa ndani!

Na kuwa naye Yesu tu, Aliye Mwokozi.

7 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page