Waumini simameni - tupeleke neno lake Neno lake Bwana Mungu - ni nuru ya ulimwengu x2 Tulisome kweli (kweli kweli) Tulihubiri sana (biri sana) Tulisambaze kote na tulifundishe kweli Tulisome kweli (kweli kweli) Tulihubiri sana(biri sana) Tulisambaze kote na tulifundishe
Ni neno la Bibilia - kutoka kwa Mungu Baba Anena kwa kinywa chake - na kwa maandiko yake x2
Ni dawa ya mioyo yetu - tulizo kwa watu wote Tulipokeeni leo - tupate kunusurika x2
Tuchezeni kwa furaha - nderemo na kwa vifijo Kwa ngoma na tarumbeta - kayamba hata vinanda x2
Milima iyumbeyumbe - miti na ichezecheze Bahari ivume sana - mito ipige makofi x2
top of page
bottom of page
Kommentare