top of page

Wakuabudiwa

Wakuabudiwa, wakuheshimiwa ni wewe

Mungu wakupewa sifa, na utukufu,

ni wewe Mungu Mungu mwenye nguvu,

wastahili heshima zote hakuna mwingine

wa kulinganishwa na wewe Mungu x2


Umesema wewe, jina lako liko liliko ni

we Mungu unafanya mambo yaliyo juu

ya fahamu zetu Mungu ukisema ndiyo,

nani awezaye kupinga? hakuna wewe

unatupa kushinda na zaidi ya kushinda

unatupandisha utukufu hadi utukufu x2


Uzima wetu uko mikononi mwako Mungu

unawapa nguvu, wanyonge na wadhaifu

Mungu unawanyeshea mvua wema

na waovu mungu wanadamu nani wa

kulinganishwa na wewe nani wenye nguvu

wa kusimama mbele yako Mungu x2

3 views0 comments

Opmerkingen

Beoordeeld met 0 uit 5 sterren.
Nog geen beoordelingen

Voeg een beoordeling toe
bottom of page