Wakristu wote simameni, simameni Tuchezeni mbele za Bwana, kwa shukrani (Leo) Asubuhi na mchana nitamsifu (Bwana) Na usiku nitaita jina la Bwana (wangu) Sifa zake zi kinywani mwangu daima nitaimba sifa zake Mungu milele
Tupeperusheni mikono juu hewani Tushangilieni tupigeni makofi
Ametulisha kwa chakula cha mbinguni Twaburudika kwa kinywaji cha uzima
Ametukinga na maovu ya dunia Mapenzi yake kwetu sisi ni ya ajabu
Turukeruke na tucheze kama ndama Tupigeni ngoma kayamba na vinanda
top of page
bottom of page
Comments