Wakati sasa umeshafika wa kujifikiria Kitu gani umtolee Bwana kama shukrani zako.
Toa kwa moyo wa mapendo, Toa ulicho nacho (Ndugu) toa kwa ukarimu Mungu anakuona ndugu mpaka moyoni mwako x2
1. Ewe ndugu usimame, nenda mbele zake Bwana, kamtolee sadaka Bwana kwa mapendo yote.
2. Tolea moyo wako, pamoja na mapendo yako naye, Bwana Mungu wako kweli atakubariki.
3. Siku zote Mungu wako, alikulinda vyema nawe sasa, ndugu yangu hima ujifikirie.
Comments