Mwimbieni Bwana wimbo ule mpya maana ametenda mambo ya ajabu.Paazeni sauti imbeni saburi tangazeni sifa zake Mungu wetu x2
Waimbaji wa Mungu- imbeni kwa shangwe, chezeni kwa furaha mbele zake Bwana. Pigeni tarumbeta -vinanda na zeze, ngoma na baragumu hata na kayamba (wote)
Mpeni bwana Mungu -enyi watu wake, mpeni utukufu mpeni na nguvu. Mwabuduni daima -kwa uzuri wake iteni jina lake kwa utakatifu (wote)
Sauti yake bwana -i juu ya maji, na tena ina nguvu inayo adhama.Yawalisha ayala -sauti ya Bwana, na wote wanasema utukufu wake (wote)
Yeye hufanya jua- liwake mchana, nao mwezi na nyota usiku wa giza. Anawalisha ndege- wote wa angani, na wote wana sema utukufu wake (wote)
Mungu ni wa upendo- amejaa huruma, rehema zake kweli hazina mpaka. Fadhili zake Bwana -zinadumu kweli, milele na milele hata na milele (wote)
Comments