top of page

Waimba Sikizeni

1. Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni;

Wimbo wa tamu sana,Wa pendo zake Bwana;

"Duniani salama, Kwa wakosa rehema."

Sisi sote na twimbe, Nao wale wajumbe;

Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni.



2. Ndiye Bwana wa mbingu, Tangu milele Mungu,

Amezaliwa mwili, Mwana wa mwanamwali;

Ametoka enzini, Kuja ulimwenguni

Mwokozi atufie, Ili tusipotee,

Waimba, sikizeni, Malaika mbinguni.



3. Seyidi wa amani, Ametoka Mbinguni,

Jua la haki, ndite, Atumulikiaye;

Amejivua enzi, Alivyo na mapenzi,

Ataka kutuponya, Kutuzalisha upya,

Waimba, sikizeni,Malaika mbinguni.

2 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page