1. Utukuzwe ewe Baba Mungu utukuzwe - aleluya Kwani Yesu mfufuka ametualika - aleluya
Utukuzwe, Utukuzwe Baba Muumba ulimwengu Aleluya aa
2. Tumepokea mkate mazao ya mashamba, ndio alama kwetu ya wema wako mkuu
4. Zawadi ya divai kutoka mizabibu - ndio alama kwetu ya wema wako mkuu -
5. Ni tunda la bidii ya mkono na ya moyo-‘jalie iwe kwetu kinywaji chake roho –
6. Sifa kwako ee Mungu kwa kutuonyesha mkate – shukrani kwako Baba kwa kutulisha sisi -
7. Utukuzwe ee Mungu uliyetuchagua – tuwe taifa lako la kukutumikia –
8. Kwa pendo na fadhili umetufurahisha – ukatufikisha kwa sherehe yetu leo –
9. Siku ya leo iwe kwa heshima na sifa - na utukufu wako na kwa mafia yetu –
Please add the missing music scores. This is really good work