Utukuzwe ee Bwana, Mungu wa ulimwengu, maana kwa wema wako, sisi twakutolea( Vipaji vyetu hivi, mkate na divai ni mazao ya nchi na kazi zetu)x2
1. Pokea zawadi tunaleta, ni shukurani kwako Bwana.
2. Pokea mazao ya mashamba, ni kazi yetu wanadamu.
3. Tunakutolea nyoyo zetu, zitakase ee Bwana Mungu.
4. Vitu vyote Bwana mali yako, twakuomba Bwana pokea.
5. Na sisi wote ni mali yako, tunajitolea kwako Bwana
Comments