Usipange foleni kwenye duka la shetani, Utauziwa dhambi faida yake mauti Nenda ukajipange dukani kwa Bwana Yesu, Utapata kibali cha kuingia mbinguni
Enyi wavuta bangi, na madawa ya kulevya Mbona mmejipanga katika duka la shetani
Na ninyi wala rushwa, makahaba na wachawi Mbona mmejipanga katika duka la shetani
Duka lake shetani limejaa vitu vingi Tena vyapendeza sana na kuuvutia moyo
Ramani ya mbinguni nenda kwake Yesu Ramani ya kuzimu shetani ndiye mchoraji
Mnaofunga ndoa katika jinsia moja Nanyi mmejipanga katika duka la shetani
Mavazi ya aibu dada zetu mwajivika Mnaita vimini shetani anachekelea
Comments