Usifiwe Utatu Mtakatifu na umoja usiogawanyika
Usifiwe Utatu Mtakatifu/ na umoja usiogawanyika.
Sisi sote tutautukuza/ kwa sababu ametufanyizia huruma yake.
Ee Bwana Mungu wetu / jina lako ni la ajabu popote duniani.
Nikiziangalia mbingu zako / kazi ya vidole vyako.
Mtu ni kitu gani hata umkumbuke / na binadamu hata umwangalie?
Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu / umemvika taji la utukufu na heshima.
Atukuzwe Baba na Mwana / na Roho Mtakatifu.
Comments