Watu wengi tunajaribu upendo Tunawajali wale wanaotuhusu Tunaojua wataweza kutulipaHatuwathamini wale wasiotuhusu wala wasiojiweza, lakini
Tunawakopesha wenye kipato kikubwa Tukiamini nao watatukopesha Wakitujia wenye shida na fukara Tunawakimbia eti hawakopesheki Na wana madeni mengi, lakini
Wakiugua wenye nafasi za juu Tunajazana kwao na vichupachupa Tukiamini na sisi tukiuguaWatalundikana kwetu na vifuko fuko Kadi na michango mingi, lakini
Tukitembelewa na mtu mwenye viraka Tunauliza kama tulimualika Akija aliyeshuka kwenye shangingi Tunamwuliza kinywaji anachokunywa Tena kwa unyenyekevu lakini
top of page
bottom of page
Comments