Uniangalie atwambia, Yesu aliyetufia;
Msalabani ni uzima, Hapa utaipata hazina.
Kutazama Kalvari, Kutazama Kalvari,
Ni kupewa kuishi Kuutazama mti wa Kalvari.
Ninapojaribiwa ghafula, Shetani hatanitega;
Nikitazama msalaba, Nguvu nitaipata kwa Bwana.
Msalaba nitautazama Kila wakati daima,
Ahadi nitategemea, Hivi kabisa sitaanguka
Comments