(Umeniita Bwana nipokee) x2 (nimeitika wito niwe mtumishi wako milele x2)
Umeniita Bwana kufanya kazi katika shamba lako: umeniongoza niwe mtumishi wako mwaminifu
Ulisema ukitaka kunifuata ukubali kuacha yote; nami nimekubali wito wako
Bila wewe mimi siwezi kitu: neno lako Bwana laniongoza
Comentarios