Tunakuja kwako Baba na maombi yetu (Baba) utusikilize Baba utuhurumie. Tazama watu – wanavyo kufa kila siku. Ugonjwa wa ukimwi unatumaliza. Ukimwi haujali lugha, ukimwi haujali taifa, ukimwi haujali rangi x2 Wazee, vijana, watoto, hao wote wanakufa
Ulimwengu wote unajiuliza juu ya ugonjwa huu, unaomaliza watu katika dunia hii, waganga wanajitahidi hawajapata madawa. (Mungu tusaidie tunakulilia x2
Ukitembelea familia nyingi katika nchi yetu, utawakuta watoto wasio na wazazi, wajane wameongezeka, hawapati msaada Mungu x2
Watu wengi bado hawajakubali kwamba ukimwi upo, lakini wafundishwa juu ya ugonjwa huu, wameshindwa kujihadhari, na ugonjwa wa ukimwi (ukimwi ni hatari watu kufa wote x2
Watu wote ondokeni tupigane na ugonjwa wa ukimwi, silaha yetu ni Mungu anayetuongoza, tufundishe wenzetu wote ili wajihadhari. (Sote tujihadhari, na ugonjwa huu x2
Comments