top of page

Uishi Ndani Yangu

Tawala ndani yangu, Ee Yesu, Mfalme.

Uwe kwangu majibu Kwa maswala yangu;

Uishi ndani yangu, Wewe, mwongozi

Utumishi ni wangu, Wako utukufu.


Hekalu nimetoa, Umelisafisha;

Sasa fahari yako Imulike ndani;

Dunia iwe kimya, Mwili sasa uwe

Mtumwa mtulivu Wa kukutii tu.


Viungo vyake mwili, Vyote vikungoja

Tayari vikiitwa Kwenda, kusimama;

Bila manung`uniko Au malaumu,

Au kusumbuliwa, Pasipo majuto.


Niwe na utulivu Pasipo haraka;

Tayari kungojea Maagizo yake.

Tawala ndani yangu. Ee Yesu, Mfalme,

Uwe kwangu majibu Kwa maswali yote.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page