top of page

Twimbe Twimbe Jamani

Tumwangalie Mkombozi,

akitundikwa masalabani; tutatambua

upenzi, aliotupenda moyoni


Twimbe, twimbe, jamani:

Salaam Yesu msalabani! x2


Msalabani sio mtiwe, tunaotoka

kuheshimu; ila ni Yesu mwenyewe, kwa

binadamu mwaga damu


Tuusifu sana mti huu, Yesu akauchagua;

kwa mapendo yake makuu deni zetu

kuzilipia.


Kwa stahimilize msalaba, twapata

msamaha wa dhambi; ni Yesu mwenye

kumuomba, Babaye Mungu wetu Rabi.


Msalaba kwa zake nguvu, Uwingu

wafunguliwa; yakoma enzi ya mwovu,

na utumwa waondolewa.

45 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page