top of page

Twendeni Wote kwa Bwana

Twendeni wote kwa Bwana, atualika

karamuni, tukale mkate wa mbingu.


Yeye mwenyewe ni Mungu, Na pia ni mwanadamu, jamani.


Yeye ni mkate halisi, Yeye ni shibe halali, jamani.


Yeye ni Mwana wa Mungu, Mtawala Mkuu wa mbingu, jamani


Yeye ni penzi la Baba, Yeye ni Neno la Baba, jamani.


Yeye ni mwanga wa kweli, Tena ni njia ya kweli, jamani


Yeye ni mpenzi wa wote, Faraja kweli kwa wote, jamani.


Yeye ni mlango wa mbingu, Tuzo na heri ya mbingu, jamani.

1 view0 comments

ความคิดเห็น

ได้รับ 0 เต็ม 5 ดาว
ยังไม่มีการให้คะแนน

ให้คะแนน
bottom of page