Twendeni wote kwa Bwana, atualika
karamuni, tukale mkate wa mbingu.
Yeye mwenyewe ni Mungu, Na pia ni mwanadamu, jamani.
Yeye ni mkate halisi, Yeye ni shibe halali, jamani.
Yeye ni Mwana wa Mungu, Mtawala Mkuu wa mbingu, jamani
Yeye ni penzi la Baba, Yeye ni Neno la Baba, jamani.
Yeye ni mwanga wa kweli, Tena ni njia ya kweli, jamani
Yeye ni mpenzi wa wote, Faraja kweli kwa wote, jamani.
Yeye ni mlango wa mbingu, Tuzo na heri ya mbingu, jamani.
ความคิดเห็น