Twende wote aste aste na sadaka mikononi vipaji mbalimbali twende wote kwa furaha, Mungu wetu tubariki Mungu wetu atuongoze na tuseme aleluya daima na milele x2
Mungu Baba tubariki Mungu mwana ‘tukomboe naye Roho Mtakatifu atuongoze daima
Sadaka zetu mikononi matoleo kwako Baba, vyote vyako Mungu wetu tubariki daima
Watoto wetu twatoa kwako kufanya kazi yako Mungu, watoto wako Mungu wetu wabariki daima
Mali yote yatoka kwako mifugo, mimea pia kwako twasema sante Mungu wetu usifiwe daima
Kaka dada usiachwe nyuma zawadi yako mikononi ili ujazwe Baraka tele kutoka kwake Mungu wetu.
Ingawa wa Baba ni kidogo pokea zawadi zetu, tumetoa kulingana na uwezo wetu
Kommentare