Tupalize sauti zetu twimbe kwa furaha, kama vile watu wote walivyomwimbia, Rabbi Yesu alipoingia Yerusalemu x2
Hossana, hosanna, hosanna, ndiwe utakaye miliki nyumba ya Daudi x2
Bass: Mbarikiwa ni mwenye kuja , All: Kwa jina la Bwana x2 Hossana, hosanna, hosanna, ndiwe utakaye miliki nyumba ya Daudi x2
(Nguo zao) kazitandika (huko njiani) Ndipo Yesu Mfalme Mtukufu apite x2
(Hata wengine) wakayakata matawi wakayatandika (huko njiani) ndipo Yesu Mfalme Mtukufu apite x2
Hossana, hosanna, hosanna, ndiwe utakaye miliki nyumba ya Daudi x2
Ajabu kuu kaonekana huko Yerusalem, Rabbi Yesu akapanda juu ya mwana punda, kwa shangwe kuu Yesu kaingia Yerusalemu x2
Hossana, hossana, hosanna, ndiwe utakaye miliki nyumba ya Daudi x2
Nasi sote tujitakase kumngoja Mwokozi, arudipo tuwe safi kuingia naye huko mbinguni ndiko Yerusalem ya milele x2
Hossana, hosanna,hosanna, ndiwe utakaye miliki nyumba ya Daudi x2
Comments