top of page

Tunakuangukia Ee Mungu

Tunakuangukia, ee Mungu , wa huruma, ondoa dhambi zetu, tugeukie tena.

  1. Nakulilia mchana kutwa, unisikie, kilio changu kikufikie, ee Mungu wangu

  2. Nifurahishe, mtumishi wako, u heri yangu, kushika amri ulizotoa nakusudia.

  3. Nategemea mwongozo wako, usiniache, mapito yako unifundishe, niwe msikivu.

  4. U peke yako Mwenyezi Mungu ndiwe uwezo, U peke yako atupendaye ndiwe upendo

  5. Anayeomba msaada kwako unamjalia, anayekusihi kwa zaburi, humwitikia.

  6. Tunapojuta makosa yetu, watusamehe, huruma yako haina mwisho, tuelekee.

0 views0 comments

Komentarze

Oceniono na 0 z 5 gwiazdek.
Nie ma jeszcze ocen

Oceń
bottom of page