Tunakuangukia, ee Mungu , wa huruma, ondoa dhambi zetu, tugeukie tena.
Nakulilia mchana kutwa, unisikie, kilio changu kikufikie, ee Mungu wangu
Nifurahishe, mtumishi wako, u heri yangu, kushika amri ulizotoa nakusudia.
Nategemea mwongozo wako, usiniache, mapito yako unifundishe, niwe msikivu.
U peke yako Mwenyezi Mungu ndiwe uwezo, U peke yako atupendaye ndiwe upendo
Anayeomba msaada kwako unamjalia, anayekusihi kwa zaburi, humwitikia.
Tunapojuta makosa yetu, watusamehe, huruma yako haina mwisho, tuelekee.
Komentarze