Enyi vijana tuandamaneni sote, tukishika MATAWI ya mitende mikononi, tumshangilie Mfalme wa Dunia yote, Bwana aliye juu, Mfalme Mkuu wetu. Tumwimbieni Hosana, Mwana wa Daudi Hosana, Ndiye Mbarikiwa ajaye, kwa jina la Bwana Hosana×2
Tutandikeni ngu-o zetu njiani, Kama walivyofanya watoto wa wae-brania, tupazeni sauti zetu tukisema: Hosana Ho-sana, Hosana juu mbinguni.
Twa- waalika nyote mjiunge nasi, tukimshangilia yeye Bwana wa majeshi, sifa twampa huku mateso aanza, Bwana ndiye Mfalme, Mfalme wa Utukufu.
Kibwagizo
Twendeni Yerusalemu, tukimshangilia Mungu wetu kwa furaha, Utukufu sifa na heshima viwe, kwa-ko Ee Kristu, Mfalme Mkombozi.
Tumwimbieni Hosana, Mwana wa Daudi Hosana, Ndiye Mbarikiwa ajaye, kwa jina la Bwana Hosana×2
Comments