Unison)Tumeingia kwako Bwana, tunaimba kwa furaha nyumbani mwako. x2 Tuko mbele zako asubuhi tumekuja
Nyumbani mwako Mungu Baba utupokee utubariki x2
Kwa shangwe kubwa vigelegele na nyimbo Baba tumekuja-hekaluni mwako. kwa vinanda kwa vinubi kwa machezo Baba tumekuja –hekaluni mwako.
Bwana ututakase sisi wanao leo asubuhi-Altareni mwako, Bwana utujalie baraka zako leo asubuhi- Altareni mwako.
Nyumba yako ni nyumba ya sala tumekuja tupokee-utusikilize. Dua zetu maombi yetu na sala zetu zipokee-utusikilize.
Nyua zake Bwana kweli zapendeza macho njooni nyote-njooni tumwabudu, ingieni malangoni mwake kwa furaha tumwabudu- leo na milele.
תגובות