top of page

Tena Mwokozi, Twalitukuza Jina Lako

Tena, Mwokozi, twalitukuza jina lako lenye kupendeza,

Twangojea neno la amani, Kabla hatujakwenda nyumbani.


Tupe amani njiani mwetu, Wewe umwanzo, umwisho wetu;

Dhambini kamwe isiingie Midomo ikutaye wewe.


Utupe amani usiku huu, Ili gizani kuwe nuru kuu.

Tulinde kwa kuwa kwako Bwana. Usiku nisawa na mchana.


Tupe amani ulimwenguni Ndiyo dawa yetu majonzini;

Na ikitwita sauti yako, Tupe amani milele kwako.

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page