Tazameni karamu ya Bwana iko mezani (mbele). Ni karamu ya upatanisho na ya amani (kwetu) x2 (Haya ndugu simama (ndugu) Ewe (mkiristu) jongea (mbele) x2 Yesu Kristu anatualika kwa chakula bora cha uzima x2)
Ndugu tazama Yesu anatualika, na wewe kwa nini moyo wako unasita, vikwazo gani vinavyo kusonga moyo, hata ukatae mwaliko wa Bwana Yesu
Hebu tazama wenzako wanvyokwenda, kwa heshima kwa upole na unyenyekevu, nyoyo zao ni safi nyuso za furaha, wanashiriki vyema karamu ya Bwana
Ewe mkristu utafiti moyo wako, kama una dhambi nenda ukaziungame, kwa nini unakuwa mtumwa wa dhambi acha dhambi tenda mema, ili uokoke
Haya shime twendeni Bwana atuita tushiriki pamoja karamu ya Bwana, waumini wote wenye mioyo safi, ni wapenzi wa karamu yake Bwana Yesu
Comments