Bwana Bwana Utuhurumie -
Bwana, Bwana Utuhurumie
Ee Bwana Ee!
Ee Bwana Ee!
Ee Bwana Utuhurumie
Kristu, Kristu utuhurumie -
Kristu, Kristu utuhurumie
Ee Kristu Ee!
Ee Kristu Ee!
Ee Kristu Utuhurumie
Bwana, Bwana….
UTUKUFU
‘Tukufu! ‘Tukukufu kwa Mungu Juu
Amani! Na amani duniani
(Kwa watu wenye mapenzi - wenye mapenzi mema) x2
A-ma-ni!
Sifa! Sisi tunakusifu
Heshima! Sisi tunakuheshimu
(Tunakuabudu - Sisi tunakuabudu) x2
He-shi-ma!
‘Tukufu! Sisi tunakutukuza
Shukrani Sisi tunakushukuru
Kwa ‘jili ya utukufu - Utukufu wako mkuu x2
Shu-kra-ni!
Ee Mungu! Ee Bwana Mungu
Ee Baba Mfalme wa mbinguni.
Ee Mungu Baba - Mungu Baba Mwenyezi x2
Ee Ba-ba!
Ee Bwana! Ee Bwana Yesu Kristu
Ee Mwana Kristu Mwana wa pekee
Mwana wa Baba - Mwanakondoo wa Mungu x2
Ee Mwa-na!
Mwokozi Mwenye kuondoa dhambi.
Huruma! Dhambi za dunia
Utuhurumie - Pokea ombi letu x2
Hu-ru-ma!
Ee Yesu Kwani ndiwe Mtakatifu
Ee Kristu Kwani ndiwe Bwana.
Ee Yesu Kristu - Ndiwe peke yako Mkuu! x2
Ee Kri-stu!
Umoja! Pamoja na Roho Mtakatifu.
Milele! Katika utukufu,
‘Tukufu wa Mungu Baba - Kristu anaishi x3
Mi-le-le
NASADIKI
Nasadiki kwa Mungu mmoja x2
Mwumba mbingu na dunia x2
Na kwa Bwana Yesu Kristu
Mwana wake wa pekee
Nasadiki kwa Mungu Baba -
Nasadiki nasadiki Mungu aliyetuumba
nasadiki nasadiki
Na kwa mwana mkombozi -
Na kwa roho wa uzima -
Alitungwa kwa uwezo wake x2
Roho mtakatifu x2
Kazaliwa na Maria
Yule mama na bikira
Akateswa kwa Pilato ndipo x2
Akasulibiwa x2
Kafa tena akazikwa
Akashuka kuzimu
Siku ya tatu kafufuka, akapaa x2
Hata mbinguni x2
Amekaa kuume kwa Mungu
Baba aliye Mwenyezi
Atakuja kuhukumu wazima pia x2
Na wafu x2
Na ufalme utakuwa
falme wake wa milele
Nasadiki kwa kanisa takatifu x2
Takatifu Katoliki Katoliki
Shirika la watakatifu
Maondoleo ya dhambi zetu
Nangojea ufufuko wa miili x2
Toka kwa wafu x2
Na uzima wa milele
Yote hayo nasadiki
MTAKATIFU
Mtakatifu Bwana Mungu wetu -
Ee Hosana juu!
Mtakatifu Bwana Mungu wetu -
Ee Hosana juu!
Mtakatifu Bwana Mungu wetu -
Ee Hosana juu!
Mbinguni - Mbinguni
Utukuzwe Bwana Mungu - Ee!
Mungu Muumba wetu - Ee!
Mbingu na dunia zimejaa - Ee! Ee! Ee!
Utukufu wako - Ee!
Ee, Ee, mbinguni - Ee,Hosana juu
mbinguni
Utukuzwe Bwana Mungu - Ee!
Mungu Mkombozi wetu - Ee!
Uliangamiza mauti ukaleta - Ee! Ee! Ee!
Uzima mpya - Ee!
Ee, Ee, mbinguni - Ee, Hosana juu mbinguni
Utukuzwe Bwana Mungu - Ee!
Mungu mfariji wetu - Ee!
Ulimtuma Roho kwetu tuwe - Ee! Ee! Ee!
Sote mwili mmoja - Ee!
Ee, Ee, mbinguni - Ee, Hosana juu mbinguni
FUMBO LA IMANI
Kristu, Kristu, Ee! - Kristu alikufa,
Kristu, Kristu, Ee! - Kristu alikufa,
Kristu! Ee Kristu, Kristu! - atakuja tena Kristu.
BABA YETU
Baba yetu uliye mbinguni
Baba yetu, Baba yetu
jina lako litukuzwe daima
Ee Baba, Ee Baba, Ee!
Baba yetu uliye mbinguni jina lako
litukuzwe daima
Ufalme wako ufike, utakalo lifanyike
duniani kama mbinguni
Baba yetu -
utupe leo mkate wetu wa kila siku,
utusamehe makosa yetu, kama
tunavyowasamehe na sisi waliotukosea
usitutie katika kishawishi lakini utuopoe maovuni
Kwani ufalme ni wako - Baba yetu
Kwani nguvu ni zako - Baba yetu
Utukufu ni wako - Baba yetu
Baba, milele, milele - hizi zote zako,
Baba!
MWANA KONDOO
Mwana Mwana kondoo wa Mungu
Uondoaye Uondoaye
Dhambi za dunia - Dhambi za dunia
Utuhurumie utuhurumie
Utujalie amani Utujalie amani
Comentarios