top of page

Taamini Nitii Pia

Namwandama Bwana kwa alilonena, Njia zangu huning`azia;

Na nikimridhisha atanidumisha, Taamini nitii pia.


Kuamini, Njiani pweke ni hii

Ya furaha kwa Yesu: Amini ukatii.


Giza sina kwangu wala hata wingu,Yeye mara huviondoa;

Oga, wasiwasi, sononeko, basi; Huamini nitii pia.


Masumbuko yote, sikitiko lote; Kwa mapenzi hunilipia;

Baa, dhara, dhiki, vivyo hubariki. Taamini nitii pia.


Mimi sitajua raha sawasawa Ila yote Yesu kumtoa:

Napata fadhili na radhi kamili, Taamini nitii, pia.


Nitamfurahia na kumtumaini, Majumbani na njia-njia;

Agizo natenda; nikitumwa hwenda, Huamini, nitii pia

2 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page