Ee Bwana (Bwana Mungu) utuhurumie (ee Bwana) ee Bwana Mungu (tuhurumie) utuhurumie (ee Bwana ee Mungu Mungu utuhurumie
Ee Yesu (Kristu) utuhurumie Ee Yesu Kristu utuhurumie
UTUKUFU
Utukufu (juu) kwa Mungu Mbinguni Na amani iwe kote duniani (tunakuabudu) Tunakusifu Bwana twakuheshimu Bwana tunakuabudu Twakutukuza Bwana twakuheshimu Bwana
Ewe Bwana Mungu Baba mfalme wa Mbinguni Tunakushukuru kwa utukufu mkuu, Mungu Baba Mwenyezi
Ewe Bwana Yesu Kristu Mwana wa pekee Mwana kondoo Mungu uondoaye dhambi, utuhurumi-e
Uondoaye dhambi zetu utusikie, Ewe uketiye kuume kwa Mungu Baba, utuhurumi-e
U pekee Bwana Mtakatifu na u Kristu Pamoja naye Roho katika utukufu, wake Mungu milele
ALELUYA
Aleluya (aleluya) aleluya (aleluya) aleluya aleluya
NASADIKI
Nasadiki (kwa Mungu Baba), nasadiki (kwa Mungu Mwana) Nasadiki (kwa Mungu Roho) nasadiki
Nasadiki kwa Mungu mmoja Baba ye-tu Mwenye-zi Nasadiki Yesu Kristu mwana wake wa pekee Nasadiki alipata mwili kwa Roho Mtakati-fu Nasadiki kazaliwa na Bikira Maria
Aliteswa alisulubiwa kwa amri ya Pnsyo Pilato Akafa na akazikwa na kushuka kwa wafu Alifufuka siku ya tatu na kupaa juu Mbingu-ni Toka huko tarudi kuhukumu ulimwengu
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu na Kanisa Katoliki Nasadiki Ushirika wao Watakatifu Nasadiki ufufuko wa miili na ondoleo la dhambi Nasadiki uzima wa milele na milele
MTAKATIFU
Mtakatifu (Bwana Mungu) Mtakatifu (wa Majeshi) *2 Mbingu na dunia zimejaa zimejaa Zimejaa utukufu wako Bwana
{Hosanna juu Mbinguni Hosanna Mbinguni juu Hosanna juu } *2 Amebarikiwa amebarikiwa yeye Yeye ajaye kwa jina lake Bwana
FUMBO LA IMANI
Yesu Kristu alikufa Yesu alifufuka Atarudi Yesu atakuja tena
AMINA
Amina (amina) amina (amina) amina amina
BABA YETU
Baba Yetu uliye Mbinguni, jina lako litukuzwe daima Na ufalme wako na ufike na mapenzi yako yatimilike Utakalo (utakalo) lifanyike (lifanyike) duniani (duniani) kama Mbinguni *2
Tupe leo na mkate wetu tupe mkate wetu wa kila siku Tusamehe na makosa yetu vile tusameheavyo wengine
Situtie vishawishini bali utuopoe maovuni Situtie vishawishini bali utuopoe maovuni
Kwa maana ufalme ni wako na nguvu pia nao utukufu Kwa maana ufalme ni wako na nguvu pia nao utukufu
MWANA KONDOO WA MUNGU
Ee Mwana Kondoo wa Mungu, Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia) Tuhurumie (tuhurumie) utuhurumie
Ee Mwana Kondoo wa Mungu, Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia) Tuhurumie (tuhurumie) utuhurumie
Ee Mwana Kondoo wa Mungu, Unayeziondoa dhambi za dunia (dhambi zote za dunia) Tupe amani (tupe amani) utupe amani
Comments