Ewe Bwana ‘tuhurumie (wote) [Ewe Bwana ‘tuhurumie Kwani sisi tuwakosefu (ewe) x 2] x 2
Ewe Kristu ‘tuhurumie
Ewe Bwana ‘tuhurumie
UTUKUFU
Utukufu kwa Mungu mbinguni, na amani kwa watu wema.
Twakusifu tunakuheshimu, twakuabudu tunakutukuza x 2
Utukufu kwa Mungu juu na amani, kwa watu wema pote duniani.
Tunakushukuru m-falme wa mbinguni mwema wapekee, mwana wake baba.
Mwenye kuondoa makosa ye-tu, utuhurumie maombi pokea.
Ku-u-me kwa Baba unapoketi, mtakatifu mku-u utuhurumie.
Pamoja na Roho M-takatifu, ndani yake Baba we’ unatukuzwa.
NASADIKI
Nasadiki Kwa Mungu mmoja
Baba mwenyezi muumba wa mbingu na nchi na vitu vyote,
(Vinavyoonekana na visivyo, na visivyoonekana) x 2
Mungu Baba ni muumba wa vyote, Yesu Kristu ni Mwana wa pekee, Maria ni mama yake kweli, aliteswa akafa sadaka.
Kafufuka siku ya tatu, alipaa huko uwinguni, Atarudi siku ya mwisho, ‘falmewake hauna mwisho.
Naye Roho ni mleta uzima, atokaye kwa Baba na Mwana, Huabudiwa pamoja naye, hunena Kwa vinywa vya manabii
Nasadiki kwa Kanisa moja, takatifu pia la kitume, Naungama ubatizo mmoja, nangojea u-zima wa milele.
MTAKATIFU
Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu Bwana Mungu wa majeshi x 2
Mbingu na dunia (mbingu) zimejaa utukufu wako x2
Hosanna, hosanna (hosanna) juu mbinguni x2
Mbarikiwa anayekuja kwa jina lake Bwana x 2
BABA YETU
Baba yetu uliye mbinguni (Baba) jina lako litukuzwe po-te, ufalme wako utufikie (Baba) utakalo Baba lifanyike x 2
Baba yetu mwema uliye mbinguni, jina lako Baba litukuzwe.
Na u-falme wako uje hapa kwetu, na mapenzi yako yatimizwe.
Tupe leo m-kate wa kila siku, utupe leo m-kate wetu.
Baba u-tusamehe makosa yetu, kama tusamehavyo we-nzetu.
Baba usituache vishawishini, ila utukinge na ma-ovu.
U-falme na nguvu nao utukufu, vyote ni vyako hata milele
MWANAKONDOO
Ewe Mwanakondoo wa Mungu
Unayeondoa dhambi zetu utuhurumie (mwanakondoo) utuhurumie x 2
Ewe Mwanakondoo wa Mungu
Unayeondoa dhambi zetu utuhurumie (mwanakondoo) utuhurumie x 2
Ewe Mwanakondoo wa Mungu
Unayeondoa dhambi zetu, utupe amani (Bwana) utupe amani, (Bwana) Utupe amani x 2
Comments