BWANA UTUHURUMIE
Bwana Bwana (Bwana) tuhurumie
Bwana Bwana tuhurumie x 2
Kristu Kristu Kristu (tuhurumie)
Kristu Kristu tuhurumie x 2
Bwana Bwana (Bwana) tuhurumie
Bwana Bwana tuhurumie x 2
UTUKUFU
Sop: U-tukufu kwa Mungu juu
KIITIKIO:Na amani duniani (duniani), kwa watu wenye mapenzi mema x 2 (Amani)
1. Tunakusifu, tunakuheshimu, tunakuabudu, twakutukuza
2. Tunakushukuru Mfalme wa mbingu, Mwana wa pekee, Mwana wa Baba.
3 .Unayeondoa makosa yetu, utuhurumie tusikilize.
4. Kuume kwa Baba, unapoketi Mtakatifu mkuu tuhurumie.
5. Roho Mtakatifu, pamoja naye ndani yake Baba, unatukuzwa
NASADIKI
KIITIKIO:Nasadiki (mimi) ninasadiki, nasadiki (mimi) ninasadiki x 2 (kweli)
1. Nasadiki kwa Mungu Baba muumba wa vyote,
Nasadiki kwa Yesu Kristu mwana wa pekee,
Kwa uwezo wa roho Mungu katwaa mwili,
Na hapo Bikira Maria akawa Mamaye.
2. Kwa amri ya Ponsyo Pilato kasulubiwa,
Akafa na akazikwa kashuka kuzimu,
Siku ya tatu kafufuka, kapaa mbinguni,
Kaketi kuume kwa Baba, Kwa Baba mwenyezi.
3. Atarudi siku ya mwisho kutuhukumu,
Nasadiki kwa Roho Mfari-ji Mtakatifu,
Kanisa pia takatifu la Katoliki,
Ushirika wa wataka –tifu wa mbinguni.
4. Na maondoleo ya dhambi kwa ubatizo,
Ufufuko nao uzima ule wa milele x 2
MTAKATIFU
Mtakatifu/Mtakatifu Mtakatifu Mungu wa majeshi, mbingu na nchi / Mbingu na nchi zimejaa utukufu wako
Hossana juu x 3 Hossana Mbinguni x 2
(S/A) Mbarikiwa (yeye) mwenye kuja kwa jina la Bwana.
BABA YETU
KIITIKIO: Baba yetu wa mbinguni jina lako (Baba) litukuzwe
(Ufalme wako utufikie duniani kama mbinguni x 2)
Ufalme wako utufikie, duniani na kama mbinguni.
Utupe leo mkate wetu, utusamehe makosa yetu.
Usitutie kishawishini, utuopoe na maovu.
Ufalme nguvu na utukufu, vyote ni vyako hata milele.
MWANAKONDOO
Mwanakondoo, Mwana wa Mungu, unayeondoa makosa yetu (Mwana) tuhurumie x 2
S/A: Mwanakondoo wa Mungu, unayendoa makosa yetu.
Wote: Utujalie amani, utujalie (Mwana) utujalie amani x 2
Comments