BWANA UTUHURUMIE
Sop: Bwana utuhurumie
Wote: Ee Bwana (T/B: Ee Bwana),
Wote: Sis tuwakosefu Bwana, twakuomba utuhurumie x 2
Kristu ‘tuhurumie kwani sisi tuwakosefu (A/T/B: Kristu, Kristu) All: Ewe Kristu utuhurumie x 2
UTUKUFU
Utukufu kwa Mungu juu na amani, kwa watu wenye mapenzi mema.
S/A: Tunakusifu, tunakuheshimu, tunakuabudu pia tunakutukuza
T/B: S-i-f-a na heshima ibada twakupa pia tunakutukuza
Alto: Tunakushukuru kwa ajili ya utukufu wako mkuu, ee Bwana Mungu mfalme wa mbinguni Mungu Baba Mwenyezi.
Sop: Ee Bwana Yesu Kristu Mwana wa pekee, Ee Bwana Mungu wa pekee, Ee Bwana Mungu Mwana Kondoo wa Mungu Mwana wa Baba.
Tenor: Mwenye kuondoa dhambi za dunia utuhurumie, ewe mwenye kuondoa dhambi za dunia pokea ombi letu, ewe mwenye kuketi kuume kwa Baba utuhurumie, utuhurumie.
Kwa kuwa ndiwe uliye peke yako Mtakatifu, peke yako Bwana peke yako mkuu Yesu Kristu, pamoja na Roho Mtakatifu katika utukufu wa Mungu Baba, Amina.
NASADIKI
Sop: Nasadiki kwa Mungu mmoja Baba mwenyezi mumba mbingu na nchi
Wote: Na vitu vyote vinavyoonekana na visivyo-onekana
Alto : Nasadiki kwa Bwana mmoja Yesu Kristu Mwana wa pekee wa Mungu.
Tenor: Aliyezaliwa kwa Baba tangu milele yote
All: Mungu aliyetoka kwa Mungu, mwanga kwa mwanga, Mungu kweli kwa Mungu kweli.
T/B: Aliyezaliwa bila kuumbwa, mwenye umungu mmoja na Baba ambaye vitu vyote vimeumbwa naye.
All: Ameshuka toka mbinguni kwa ajili yetu sisi wanadamu na kwa ajili ya wokovu wetu.
S/A : akapata mwili kwa uwezo wa Roho Mtakatifu,
All: kwake yeye Bikira Maria akawa mwanadamu.
S/A: Akasulibiwa pia kwa ajili yetu sisi akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato akafa akazikwa.
Wote: Akafufuka siku ya tatu ilivyoandikwa, akapaa mbinguni ameketi kuume kwake Baba, atakuja tena kwa utukufu
kuwahukumu wazima na wafu nao ufalme wake hautakuwa na mwisho.
S/A: Nasadiki kwa Roho Mtakatifu,
All Bwana mleta uzima
S/A Atokaye kwa Baba na mwana,
All Anayeabudiwa na kutukuzwa
A/T Pamoja na Baba na mwana,
All Aliyenenwa kwa vinywa na manabii.
T/B: Nasadiki kwa Kanisa moja,
All Takatifu Katoliki la mitume, naungama ubatizo mmoja kwa maondoleo ya dhambi, nangojea na ufufuko wa wafu na
uzima wa milele ijayo Amina.
FUMBO LA IMANI
Kristu alikufa, Kristu alifufuka, Kristu atakuja tena.
BABA YETU
Baba yetu wa mbinguni, Jina lako Baba litukuzwe, ufalme wako ufike (na) utakalo pia lifanyike x 2
1. Baba yetu uliye mbinguni jinalo litukuzwa, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike, duniani kama mbinguni.
2. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe waliotukosea na sisi.
3. Usitutie kishawishini, lakini utuopoe maovuni x 2
4. Kwa kuwa ufalme ni wako, nguvu na utukufu hata milele.
MWANAKONDOO
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia utuhurumie x 2
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia utujalie amani, utujalie amani, utujalie amani x 2
Utujalie, utujalie (amani) utujalie amani.
Commenti