Sitawaacha kama yatima niendapo mbinguni, Roho Mungu atawashukia. Wala msiwe na huzuni, naapa hakika, Roho Mungu atawafariji- Atawapa nguvu mioyoni mwenu, hakika atawafanya Tazama nitarudi kwake Baba mwenyezi, mda wangu wakuishi duniani umekwisha, nayo kazi yangu nimekwisha kamilisha
Tazama nitarudi kwake Baba mwenyezi , kwa kuwa yanipasa kutayarisha makao mtakapokuja mtapata yako shwari.
Tazama nitarudi kwake Baba mwenyezi, nitamsihi kweli amtume Roho wake, Roho wake Mungu apate kuwafariji.
Tazama nitarudi kwake Baba mwenyezi , nipate mamlaka ya mbingu na dunia tuzo langu pia nipate kulipokea.
Commentaires