Siku ya ubatizo wangu, nilimuahidi Mungu, nitamfuata Yesu Kristu, ndiye uzima kweli dini ya kweli neema kuu nitaishika hio tu, milele siikani
Mbali shetani akimbie, si mtumwa wake tena, nadhiri yangu niishike, nitashindana vyema, adui mbaya namkataa, furaha zake na tamaa, milele simfuati
Yesu Mkombozi yumo hapa, kwa mwili na kwa damu, Ye mwana wa mwenyezi Baba na pia mwanadamu, naiamini sii kuu, sababu ya Imani tu, milele nisadiki
Yesu mchungaji anijia, miye maskini dhaifu, nguvu apate kunifia, kwa mkate mtakatifu, namtumaini yeye tu, nampenda kwa shukrani kuu, milele nitamsifu
top of page
bottom of page
Comments