top of page

Siku hii ndiyo aliyoifanya Bwana x2 Mungu (tutashangilia (na) kuifurahia (siku) tutashangilia na kuifurahia) x2

  1. Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake ni za milele, Israeli na aseme sasa, ya kwamba fadhili zake ni za milele.

  2. Mkono wa kuume wa Bwana umetukuzwa, mkono wa kuume wa Bwana hutenda makuu, sitakufa bali nitaishi, nitayasimulia matendo yake Bwana

  3. Jiwe waliloli-kataa waashi, limekuwa jiwe kuu tena la pembeni, neno hili limetoka kwa Bwana, nalo ni ajabu machoni machoni petu

0 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page