Tunatoa shukrani zetu kwako, msaada wetu (Aliyeumba mbingu na dunia x2)
Ewe Bwana mavuno haya atakaye yala ajaliwe salama ya roho ya mwili
Ukikula na ukishiba utamshukuru Bwana Mungu muumba wako kwa uhai
Usiseme moyoni mwako, nguvu zangu mimi zimenipa utajiri huo bali Mungu
Tuyakinge na kuhifadhi tuliyoyapata mahitaji ya mwaka mzima twashukuru
コメント