Ni furaha Yesu kafufuka mkombozi wetu kashinda mauti x2 Utukufu sifa na heshima (kweli)ni kwake yeye kashinda mauti x2
Kweli Bwana Yesu amefufuka mzima, kwani kaburini hayumo tena, amefufuka alivyosema natufanye sote ni shangwe
Naye malaika akawatokea, wale kina mama pale kaburini, kawauliza mbona mwamtafuta, al'e hai kati ya wafu
Akawatokeya watumishi wake, wakiwa bado wamejazwa na hofu, akawaambiya amani iwe kwenu, kawajaza Roho Mtakatifu
Kumbukeni Yesu alivyosema,l ivunjeni hili hekalu lake Mungu, nami nitalijenga kwa siku tatu, kwa hakika kayatimiza
Comments