Uje Roho mtakatifu, tuangaze toka Mbingu, roho zetu kwa mwangao
Uje Baba wa maskini, uje mtoa wa vipaji, uje mwanga wa mioyo.
Ee mfariji mwema sana, ee rafiki mwanana, ewe raha mstarehe.
Kwenye kazi upumziko, kwenye joto burudisho, u mfutaji wa machozi
Ewe wanga wenye heri, uwajaze waamini, neema yako moyoni
Bila nguvu yako wewe, mwanadamu hana kitu, kwake yote yana kosa
Osha machafuko yetu, panyeshee pakavu petu, na kuponya majeraha
Ulegeze ukaidi, pasha moto ubaridi, nyosha upotovu wote
Wape waamini wako, wenye tumaini kwako, paji zako zote saba
Wape tuzo ya fadhila, wape mwisho bila ila, wape heri ya milele
Amina aleluya, amina aleluya, amina aleluya
top of page
bottom of page
Bình luận