Sasa ni wakati mzuri twendeni madhabahuni, Tukatoe sadaka zetu, tulijenge kanisa la Mungu, (Ewe ndugu yangu mkristu, Changamka, changamka, peleka sadaka kwa Bwana Nenda katoe kwa moyo mweupe uzipate baraka za Mungu) x2
Mkristu kutoa sadaka, Ndio wajibu wa kila mmoja, Hivyo mkristu kumbuka wajibu, Nenda katoe sadaka kwa Bwana.
Mwambie Bwana Mungu wako, Baba pokea nilichokileta, Hiki ndicho ulichonijalia, Nakutolea kama shukrani.
Zamani za mababu zetu, Walipeleka sadaka za nyama, Nasi wakristu wa leo twendeni, Tupeleke fedha za mifukoni.
Comments