1. Sasa ndio wakati wa kutoa sadaka, kila mtu aanza kujifikiria
Toa ndugu, toa ndugu x2, ulicho nacho wewe, Bwana anakuona mpaka moyoni mwako.
2. Wiki nzima Bwana Mungu alikulinda vyema , sasa nawe ndugu yangu ujifikirie.
3. Kumbuka jinsi Yesu alivyojitolea pale msalabani kwa ajili yetu.
4. Tolea moyo wako, pia matendo yako, naye Bwana Mungu akubarikie.
5. Baraka zake Mungu, za Baba na za Mwana, za Roho Mtakatifu zikae nanyi nyote.
Comments