Sasa ndio wakati wa kutoa sadaka, Kila mtu aanze kujifikiria Zilete zilete, zilete kwa Bwana Zilete zilete zilete kwa Bwana
Tolea moyo wako, pia matendo yako, Naye Bwana Mungu wangu, atakubariki
Wiki nzima Bwana Mungu, amekulinda vyema, Sasa nawe ndugu yangu, ujifikirie
Kumbuka jinsi Yesu, alivyojitolea, Pale msalabani, kwa ajili yako
Baraka zake Mungu, za Baba na za Mwana, Na za Roho Mtakatifu ziwe nanyi nyote
top of page
bottom of page
Comments