top of page

Pokea Shukrani


  1. Jua linapochomoza jua ni ishara Mungu atupenda sana, kwani (kwani ni dhahiri) ni dhahiri tumeiona (ona ona siku) siku, tumtukuze Mungu daima Tumwimbie siku zote tumwabudu kila siku ni yeye (Mungu) pekee (yake) tumpe sifa Ni Mungu wetu (upokee sifa) pokea sifa kwa pendo lako pokea shukrani, watupenda he he pokea sifa (kwa pendo lako) pokea shukrani ,wewe baba (upokee sifa) pokea sifa kwa pendo lako pokea shukrani, unatujali he he pokea sifa kwa pendo lako pokea shukrani

  2. Hewa safi tunayopumua ni zawadi ya thamani kubwa sana Mungu (Mungu tujalia) katujalia bure (bila ya malipo) bila malipo

  3. Sisi tunatoa shukurani kwako Mungu kwa mema umetutendea

  4. Wewe ni mwema sana, pia wewe ni mkuu, tumtukuze Mungu daima Twakumiminia, sifa zipokee Mungu wetu, sifa ni zako, milele zipokee Mungu wetu, enzi nguvu, utukufu upokee Mungu wetu, vyote ni vyako, ee baba upokee Mungu ee twakupa (Mungu) sifa twakupa (pia) na nguvu, twakupa sifa na nguvu, Mungu pokea, twakupa (tena) sifa twakupa (pia) na nguvu twakupa sifa na nguvu, Mungu pokea sifa, pokea sifa, pokea sifa, pokea sifa Wewe ni alfa na omega Mungu upokee sifa Wewe ni mwanzo pia mwisho Upokee sifa Unatawala mbingu na nchi Mungu upokee sifa Milele uhimidihiwe Mungu pokea shukrani

10 views0 comments

Comments

Rated 0 out of 5 stars.
No ratings yet

Add a rating
bottom of page